Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ben Pol afufua penzi la Ebitoke

Alhamisi , 9th Aug , 2018

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye ilisemekana yupo kwenye mahusiano ya kimapenzi na muigizaji wa vichekesho Ebitoke, ameweka wazi juu ya mahusiano yao kwamba walishindwa kuwa wapenzi kutokana na mmoja wao kutokuwa muwazi kwa mwenzake.

Ben Pol amebainisha hayo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa mubashara kupitia ukurasa wa kijamii wa facebook wa EATV, baada ya miongoni mwa shabiki zake waliokuwa wakimfuatilia, alipotaka kufahamu undani wa mahusiano yake na Ebitoke.

"Kiukweli sijawahi kuwa na mahusiano na Ebitoke na wala ile haikuwa kiki. Kilichotokea ni kwamba hatukufanikiwa kuwa na mahusiano licha ya wananchi au mashabiki zangu wenyewe kumpitisha kuwa mpenzi wangu kabla ya mimi sijamuona na kumkubali", amesema Ben Pol.

Pamoja na hayo, Ben Pol ameendelea kwa kusema "Ebitoke alikubarika hadi kwa wazazi wangu kutokana na yeye kuonekana kwenye vyombo vya habari akidai mimi ni mpenzi wake. Wazazi wakawa wanajua kwamba wameshapata mkwe wao. Hapakuwa na mapenzi ya kweli baina yetu ila tulikuwa tunafanya vile ili kuwaridhisha mashabiki zetu".

Mbali na hilo, Ben Pol amesema chanzo cha mapenzi hayo kushindwa kuendelea ni kutokana na Ebitoke kuogopa kusema ukweli.

Kati kati ya mwaka 2017, Ebitoke kwa mara ya kwanza aliweka hadharani hisia zake za kimapenzi juu ya msanii Ben Pol, lakini kwa bahati mbaya alishindwa kueleweka kwa haraka kwa jamii, kutokana na muonekano wake ambao watu walimzoea kumuona na kupelekea kudharauliwa huku wengine wakimshauri atafute mwanaume wa aina yake.

Juni 25 mwaka 2017, Ben Pol kupitia mitandao ya kijamii alimwagia sifa Ebitoke ikiwa kama ishara ya kukubali ombi la mwanadada huyo kuwa naye kimahusiano licha ya kuwa ukweli wa kila kitu walikuwa wanaufahamu wenyewe.

Mtazame hapa chini Ben Pol akifunguka mengine zaidi..

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa