Jumapili , 29th Jun , 2014

Msanii wa miondoko ya RnB nchini Ben Pol amezungumzia kuhusu mauzo ya nyimbo zake kupitia mitandao yaani Online ambapo baadhi ya wasanii wengi nchini wamekuwa wakijiunga na kuuza kazi zao kupitia njia hizo.

Msanii wa RnB nchini Ben Pol

Ben Pol amezungumza na enewz akielezea faida na pia ni jinsi gani ambavyo amenufaika kwa kuuza album zake japokuwa bado zoezi hilo linaonekana kuwa gumu kulingana na soko lilivyo kwa sasa katika sekta hiyo nchini.