Ijumaa , 15th Jan , 2016

Kutokana na kukaa kimya kwa muda mrefu, staa wa Bongofleva Bob Junior ameeleza kuwa amekuwa akihofia kutoa kazi toka mkusanyiko wa rekodi nyingi alizonazo kutokana na kuhofia kutokuwatosheleza mashabiki zake.

staa wa Bongofleva Bob Junior

Yote haya kutoka kwa staa huyo ni kwamba anataka kurejea kama Bob Junior mpya katika gemu ya muziki inayobadilika kwa kasi kubwa.

Bob Junior ameieleza eNewz kuwa, amefanya kazi kubwa kabisa ambayo anatarajia kutoka nayo mwezi ujao akiamini kuwa itamrudisha katika nafasi yake, hapa mwenyewe akivunja ukimya wake kupitia mahojiano tuliyofanya naye, kubwa kutoka kauli yake likiwa ni hofu na kujipanga kutosheleza mashabiki kwa rekodi kali.