Jumanne , 22nd Jun , 2021

Msanii wa filamu Niva Supa Marioo amesema BongoMovie wanajipanga kuweka kambi Wilaya ya Rorya mkoani Mara ambapo msanii mwenzao Juma Chikoka maarufu Chopa Mchopanga ameteuliwa kuwa Mkuu wa wilaya hiyo.

Msanii Niva Supa Marioo

"Shukrani kwa Rais Samia kwa kutukumbuka wasanii, kila siku tunaona ma DC wanatokea Polisi au Usalama lakini safari hii ametukumbuka sisi na BongoFleva na hajapendelea".

"Wilaya ambayo ndugu yetu yupo tunaenda kutia kambi kumsapoti kama wiki na kuitangaza wilaya yake watu wajiandae, tunapekeka Vibe hata kama kijijini patakuwa mjini kwa dakika sifuri" amesema Niva Marioo 

Chopa Mchopanga na ameapishwa na Mkuu wa mkoa wa Mara Ally Hapi na tayari ameshaanza kazi katika wilaya hiyo.