Jumapili , 19th Apr , 2026

Super star wa muziki Africa Davido amemtaja Chris Brown kuwa ndio msanii pekee wa kimataifa anayesapoti muziki wa Afrobeats kwa dhati kabisa tangu siku ya kwanza.

Picha ya Davido na Chris Brown

Davido anasema Chris Brown ameunga mkono Afrobeats, amejitokeza kwenye shows zao, anarekodi nyimbo na wasanii hao kabla muziki huo haujawa mkubwa kimataifa.

Ikumbukwe Davido na Chris Brown ni marafiki wakubwa ndani na nje ya muziki wanaoufanya na pamoja wameshafanya zaidi ya nyimbo 5.