Jumatatu , 23rd Jun , 2014

Mrembo Diana Festo ndiye amebuka mshindi wa taji katika Shindano kubwa kabisa la Nice and Lovely Miss Tanga 2014, sambamba na zawadi nono ya Gari aina ya Vits.

Miss Tanga 2014 Diana Festo

Shindano hilo limefanyika kwa mafanikio makubwa katika mchuano mkali kabisa wa warembo 14, ambapo pia mrembo Noon Juma ndiye aliyeshikilia nafasi ya pili, akifuatiwa na Vanessa Charles katika nafasi ya tatu na kutoka Tanga Mkonge Hotel, hivi ndivyo mambo yalivyokuwa.

Shindano hili lililoongozwa vyema na MC, Mtangazaji mahiri wa EATV Deogratius Kithama, lilihudhuriwa na ugeni mzito wa Mkuu wa wilaya ya pangani Hafsa Mtasiwa, kama mgeni rasmi pamoja na kutiwa nakshi na burudani kutoka kwa Malkia wa Mipasho Bi. Khadija Kopa.