Picha ya Harmonize feki
Jamaa huyo ambaye jina lake halijajulikana, amechezea kichapo hicho mbele ya waandishi wa habari huku mwanamke huyo akiwa amemkunja shingoni, huku akimuuliza kwanini amemdanganya kuwa yeye ni Harmonize katika mtandao wa Instgram.
Katika utetezi wa jamaa huyo alisikika akisema "Muonekano ni kama hivi unavyouona ni fresh tu, mimi nafanana na Harmonize sijifananishi bali nafananishwa na watu ausio ila nampenda sana".
Aidha wakati huo mwanamke huyo alikuwa anampiga kichwani huku amemkunja na kumuuliza "Kwanza usiniguse wewe una Corona, ongea vizuri kwanini umeamua kunidanganya wewe ni Harmonize na ukanitongoza Instagram".