Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Harmorapa hana pesa ya kunilipa - Juma Nature

Jumanne , 28th Mar , 2017

Mkongwe wa bongo fleva Juma Kassim Nature 'Sir Nature' amekanusha vikali kulipwa na msanii Harmorapa katika wimbo wa 'Kiboko ya mabishoo' na kudai kwamba kijana huyo hana pesa za kumlipa na kusisitiza yeye alifanya kwa upendo tu.

Nature, Harmorapa

Akizungumza na eNewz ya EATV, Nature amesema kwamba alikubali kushiriki katika wimbo huo kwa sababu anaamini msanii huyo chipukizi ana uwezo mkubwa ikiwa ni pamoja na kuamini atafika mbali.

"Nikisema nimemlipisha Harmorapa pesa kwa ajili ya kolabo nitakuwa nakosea, mimi ni mtu mzima nilikubali kufanya wimbo na msanii yule kwa sababu ni mkali na anajua muziki pia na imani atafika mbali, hawezi kunilipa mimi, ana hela gani" - Juma Nature.

Katika hatua nyingine Nature kutoka TMK amesema yeye ameshakuwa mkongwe hivyo vijana kama kina Harmorapa wanapotokea kwenye ‘game’ inamlazimu kutoa sapoti ili hata watakapoondoka kuwe na watu wa kuendeleza muziki.

Aidha Nature amekanusha kusikia taarifa ambazo Harmorapa alidai kuwa amemlipa Nature kwa kolabo na kuongeza hizo taarifa kwa upande wake hazimkufikia rasmi.

Hata hivyo Harmorapa aliwahi kunukuliwa akisema siyo busara kwa wasanii wakongwe kuwalipisha pesa wasanii wachanga kwa kuwa ndiyo kwanza wanaanza kutafuta pa kutokea na kuweka wazi kuwa kwa upande wake alilazimika kumnunulia nguo Nature za kufanyia video ya ‘Kiboko ya Mabishoo’.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa