Jumanne , 25th Aug , 2015

Baada ya kukamata chati mbalimbali na ngoma yake inayokwenda kwa jina 'Hawajui', staa kinda wa michano M-Rap ameweka wazi kuwa kazi hiyo imeanza kumfungulia milango ya mikataba minono, sambamba na kumuongezea mashabiki kwa wingi.

Mkali wa michano nchini Tanzania M-Rap

M-Rap ambaye yupo mbioni kutia wino mkataba na menejimenti mpya atakayoiweka wazi hivi karibuni, amesema kuwa, kazi yake hiyo imemuwezesha kusaini mkataba na kampuni kubwa, akiwa pia na mpango wa kuiingiza katika vituo vya kimataifa hivi karibuni.