Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Iga Tena' siyo dongo kwa mtu yeyote - Msaga Sumu

Jumamosi , 22nd Oct , 2016

Mkali wa muziki wa uswazi, anayejiita 'Mfalme wa Uswahili' Msaga Sumu amesema ngoma yake mpya aliyoipa jina la 'Iga Tena' siyo dongo kwa mtu yeyote, bali ni ujumbe wa kawaida unaotokana na maisha kila siku ya watanzania.

Msaga Sumu, akiwa ndani ya FNL

Msaga Sumu ambaye amejitambulisha katika game kupitia muziki wa singeli ametoa ufafanuzi huo wakati akiitambulisha rasmi video ya wimbo huo, kupitia kipindi cha FNL, cha EATV, na kuongeza kuwa huo ni ujumbe kwa watu wote ambao wamekuwa na kawaida ya "kukopi" vitu vya watu bila kuumiza vichwa wala kutambua kazi ya muanzilishi.

Akizungumzia video hiyo, Msaga Sumu amesema ameamua kuwa serious katika muziki na ndiyo maana amefanya kitu kikubwa zaidi katika video hiyo ambayo ameonesha mazingira halisi ya uswahilini.

Kuhusu yeye kufunikwa na baadhi ya wasanii wa singeli walioshika chati hivi sasa, Msaga Sumu ameendelea kusisitiza kuwa yeye ndiye baba wa muziki wa singeli na hakuna mtu atakayeweza kumfunika.

Amesema ameitoa mbali singeli tangu enzi za vigodoro kiasi cha kutishiwa kupelekwa mahakamani na baadhi ya wasanii wa taarab, kwa madai kuwa alikuwa akitumia muziki wao, na kuingiza sauti yake.

"Mimi ndiye mwanzilishi wa singeli, nimeipigania sana toka enzi za vigodoro kabla havijapigwa marufuku, nilikuwa na loop beat za taarabu hadi akina Mzee Yusuph wanataka kunishtaki, nimepigana hadi leo hii imefikia hapa" Amesema Msaga Sumu.

Katika hatua nyingine amedai kuwa yeye ndiye aliyekiibua kipaji cha Shlo Mwamba kwa kumpa nafasi katika kazi zake

"Nilikuwa nikipata kazi nashirikisha wanagu kibao ili nao waonekane, nakumbuka kwa mara ya kwanza mimi ndiye nimemtambulisha Sholo mwamba, nilikuwa na kazi fulani, nikampigia simu, akaja, nikampa nafasi akashika kipaza akafanya mambo, na watu wakaanza kumjua"

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi