Ijumaa , 25th Dec , 2020

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) Godfrey Mngereza amefariki dunia usiku siku ya Disemba 24, huko Jijini Dodoma katika Hospitali ya General ambapo alikuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Godfrey Mngereza wa pili kutoka kushoto, baada ya kufanya interview kwenye kipindi cha PlanetBongo

Taarifa hizo zimethibitishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya BASATA ambaye ametangaza kifo hicho na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt Hassan Abbasi ambapo ameshea ujumbe wa mwisho aliotumiwa na Godfrey Mngereza kabla ya kufariki.

"Nimelazwa General hapa Dom ila kila kitu kitaenda sawa kuhusu tamasha napambana, ni meseji ya mwisho niliyoipokea juzi Jumanne saa tano na dakika 2 usiku kutoka kwa kaka yangu Godfrey Mungereza, Katibu Mtendaji wa BASATA, leo hatunaye tena katika dunia hii ametutoka, tumuombee sana mola ampe pumziko la amani la milele" ameandika Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt Hassan Abbasi 

Ratiba ya mazishi bado haijatolewa ila tunaendelea kufuatilia kwa ukaribu kukupa kile kinachoendelea kuhusiana na msiba huu.