Jumatatu , 17th Nov , 2014

Mwimbaji nyota nchini Lady Jaydee yupo katika matayarisho makubwa nchini Afrika ya Kusini kushoot video ya wimbo wake mpya alioubatiza jina 'Forever' alioshirikiana na mdogo wake Dabo.

wasanii Lady Jaydee na mdogo wake Dabo katika pozi huko Afrika ya Kusini

Wawili hao wametuma picha za pamoja wakiwa wanafanya maandalizi ya kukamilisha kichupa hicho kipya ambacho kinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu ambapo wimbo huo umefanyika Combination Sounds kwa Man Water.

Mashabiki na wadau wengi wanahamu ya kuona kolabo ya ndugu hao wawili ambayo itakuwa ni ya kwanza kuwahi kufanyika.