Ijumaa , 5th Sep , 2014

Maandalizi ya Onyesho kubwa kabisa la Kilimanjaro Music Tour, yamefikia hatua nzuri kabisa kuelekea kukamilika tayari kwa kuwapatia wapenzi wa burudani nafasi nzuri ya kufurahia muziki wa kikwao.

maandalizi ya Tamasha la Kilimanjaro Music Tour 2014, Leaders Club.

eNewz leo imefika katika eneo la tukio, Leaders Club Kinondoni na kujionea shughuli za kuweka mambo sawa tayari kwa onyesho hili na pia kuzungumza na baadhi ya wadau kuhusiana na namna walivyojianda kwa shughuli hii nzito ya Burudani hapo Jumamosi.