Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Majibu ya Stamina kuhusu ndoa za mastaa kuvunjika

Alhamisi , 16th Jan , 2020

MwanaHipHop Stamina, ametaja moja kati ya vitu ambavyo vinafanya ndoa za mastaa kutodumu ni kutopata mpenzi wa kuwavumilia kwa muda mrefu, kutokana na shughuli zao wanazozifanya.

Picha ya mwanaHipHop Stamina

Akizungumza na EATV & EA Radio Digital, Stamina amesema ndoa zinakutana na changamoto nyingi, hali inayopelekea kuvunjika kwa sababu hawapati watu waelewa na wavumilivu.

"Ukiniuliza mimi nitakwambia kitu kingine kinachosababisha ni akili zetu zenyewe, unajua shughuli za wasanii ni kutoka hapa na pale, kupata mtu ambaye atakuvumilia kwa muda wote lazima mtu awe ana uelewa na kazi yako unayoifanya, changamoto za wasanii zinajulikana leo unaweza ukawa Mwanza, kesho Dodoma kwa hiyo lazima upate mtu atakayekuelewa" Ameeleza Stamina.

Aidha msanii huyo wa HipHop ameongeza kwa kusema "Inatakiwa kuwe na viwango vya kuelewa na kuheshimu kazi ya mwenziye, kama haitakuwa hivyo utasikia mara leo katembea na huyu, kesho amechepuka na mwingine, mambo ni mengi na ndoa ina vitu vingi na kwa namna moja au nyingine nimepata nafasi ya kujifunza" ameongeza.

Stamina anatamba na wimbo wake wa asiwaze, ambapo amezungumzia mambo ambayo yamemkuta kwenye ndoa hadi kupelekea kuvunjika kwa ndoa hiyo, iliyodumu kwa muda wa mwaka mmoja.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya