Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Malkia wa Soul afariki Dunia

Alhamisi , 16th Aug , 2018

Malkia wa muziki wa aina ya 'soul', Aretha Louise Franklin kutoka nchini Marekani amefariki dunia hii leo akiwa na umri wa miaka 76, kutokana na ugonjwa uliokuwa unamsumbua wa saratasi.

Malkia wa muziki wa aina ya 'soul', Aretha Louise Franklin

Aretha ambaye ni mama wa watoto wa nne, amezaliwa mnamo Machi 25, mwaka 1942 ambapo alianza kujihusisha na masuala ya muziki kipindi alipokuwa anaimba injili katika kanisa la New Bethel Baptist lilipo Detroit mjini Michigan nchini humo.

Alipofikisha umri wa miaka 14 aliingia studio kwa mara ya kwanza kwa lengo la kurekodi muziki wake, lakini kwa bahati nzuri kipaji chake cha kuimba hakikuweza kufichika na hatimaye aliweza kuingia mkataba na moja kati ya 'lebel' kubwa za muziki duniani Atlantic Records mnamo mwaka 1966.

Mwaka 1968, alijipatia umaarufu mkubwa barani Ulaya na Marekani akifahamika kama 'Lady Soul' ambapo pia mwaka huo huo alitokea kwenye jarida la Time na kutunukiwa tuzo maalum na kiongozi wa harkati za watu weusi Martin Luther King.

Katika miaka ya 80, Aretha alitoa vibao vikali kama 'who's zooming who' na kile alichoimba na mwanamuziki wa Uingereza George Michael kiitwacho, 'i Knew you were waiting (For Me).

Mwaka 2005, alitunukiwa tuzo ya 'Presidential Medal of Freedom' na Rais George W Bush, kutokana na ushawishi wake kwa mamilioni ya wamarekani.

Katika maisha yake ya muziki, Aretha alifanikiwa kunyakua tuzo 18 za Grammy pamoja na kuwa mwanamke wa kwanza kupewa heshima ya kuwa kwenye orodha ya 'Rock And Roll Hall of Fame'.

Novemba mwaka 2017, Aretha alifanya tamasha lake la mwisho la burudani  lililokuwa lenye lengo ya kuchagia mfuko wa Ukimwi wa mwanamuziki wa nchini Uingereza Sir. Elton John.

Wanamuziki wengi duniani wametuma salaam zao za rambirambi wakiongozwa na Sir Elton John, ambaye kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika; 'kifo cha Aretha Franklin ni pigo kwa kila mtu anayependa muziki, pole nyingi kwa ndugu, rafiki na jamaa'.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali