Jumapili , 10th Apr , 2022

Mr PKP Ommy Dimpoz anasema amepokea ujumbe kutoka kwa Mama mmoja akimuomba amuoe binti yake ili aweze kumsitiri mtoto wake.

Picha ya Ommy Dimpoz

Ommy Dimpoz amefunguka kwamba "Leo nimepokea ujumbe nimecheka kweli, kuna Mama amejitambulisha na kuniambia ana binti yake mzuri na ana umbo zuri anaomba nimsitiri".

Ommy Dimpoz ameongeza kusema hataki kuoa sasa hivi kwa sababu ataonekana ameolea kupikiwa uji na futari kwenye mwezi wa Ramadhan.