Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mapenzi yake kwa mama yamuua

Jumatatu , 14th Mei , 2018

Ikiwa dunia imetoka kuadhimisha siku ya mama duniani hapo jana May 13, nakuletea historia fupi ya namna msanii ambaye alikuwa na mapenzi ya kupitiliza kwa mama yake alikubali kutoa uhai wake kwa ajili yake.

Anaitwa Garnet Damion Smith maarufu kama Garnet Silk, mwanamuziki wa reggae na mfuasi wa Rastafarai kutoka Jamaica, aliyezaliwa April 2, 1966 huko Machester Jamaica, alizaliwa na kulelewa na familia ya mama mmoja anayeitwa Etiga Gray akiwa na kaka zake na dada zake, huku akijihusisha na muziki akiwa na miaka 12 tu, na mpaka kuja kupata umaarufu mkubwa nchini Jamaica na duniani, kwa ngoma zake kali kama Love Is the Answer, Lord Watch Over Our Shoulders, Greensleeves na nyinginezo

Siku moja alikwenda kumtembelea mama yake nyubani kwao akiwa ameazima bastola kutoka kwa mwanasheria wake huku akiwa hajui namna ya kuitumia, baada ya nyumba yao kuvamiwa na vibaka, wakiwa wamekaa na rafiki zake nyumbani kwa mama yake Garnet, rafiki yake mmoja alimuomba amuonyeshe namna ya kuitumia, na kwa bahati mbaya ililipua mtungi wa gesi na kulipua nyumba yote.

Wakati moto unaendelea kuteketeza nyumba walifanikiwa kutoka nje, yeye pamoja na kaka zake na watu ambao walikuwa hapo, baada ya kugundua kuwa mama yake hajatoka nje na amebaki ndani, ndipo Garnet alikimbilia ndani kujaribu kumuokoa mama yake, lakni hakufanikiwa na wote wawili kufa kwenye ajali hiyo ya moto, iliyotokea mnamo Desemba 9, 1994.

Na huo ndio ukawa mwisho wa maisha yake na kuacha historia kubwa yenye ujumbe mzito wa namna ya upendo aliokuwa nao kwa mama yake, ulivyoweza kuondoa uhai wake, huku akiwa ameacha rekodi maalum ambayo alikuwa amemuimbia mama yake “Mama”, kutofanikiwa kumpa mama yake kama zawadi, kwani alikufa bila kusikia alichomuimbia.

Usikilize hapa wimbo wake wa 'mama'.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa