Jumapili , 22nd Feb , 2015

Maziko ya aliyekuwa staa wa muziki wa Bongo Flava, Marehemu Mez B yanatarajiwa kufanyika siku ya kesho katika makaburi ya Muhanga maili Mbili huko Dodoma

Marehemu Mez B

Maziko hayo yatafanyika baada ya taratibu za ibada na kuaga mwili, shughuli ambayo itafanyika Nyerere Square kuanzia majira ya saa nne asubuhi.

Mpaka sasa ndugu jamaa, marafiki wadau na wasanii wa muziki wameendelea kukusanyika nyumbani kwa marehemu Maeneo ya Kisasa kwaajili ya kutoa faraja na taratibu nyingine za msiba, tayari kwa kushiriki katika maziko siku ya kesho.