Happy Mushi akiwa kwenye bajaji yake
Akipiga stori na EATV & EA Radio Digital, Dada Bajaji amesema ana muda wa mwaka mmoja tangu aanze kazi hiyo ya udereva na ndoto zake ni kumilikia bajaji yake mwenyewe na kusaidia familia yake.
"Kazi ya bajaji niliona itaniingizia kipato na kukidhi mahitaji yangu ndiyo maana nikaingia, kuna mtu nilikuwa namlipa ili kunifundisha, mwanzo walikuwa wananiogopa walidhani sitakuwa serious, kwa sasa mwanaume ambaye atataka anioe aniweke ndani simtaki atakuwa anaharibu kipaji changu cha kutafuta pesa" ameeleza Happy Mushi
"Abiria wangu wakipanda hii bajaji ni maswali mwanzo mwisho na huwa nawajibu, sishangai watu wanavyonishangaa kwa sababu kwetu Tanzania inajulikana kazi ya bajaji ni ya wanaume ila nataka niwatoe mshangao wao sasa hivi wameanza kunizoea" ameongeza
Maongezi zaidi tazama hapa chini kwenye video.