
Picha ya msanii Amber Rutty
Taarifa hiyo imetolewa kwenye barua waliyoichapisha Halmashauri ya Manispaa ya Temeke kwenda kwa vyombo vya habari kuhusu kukanusha ugeni huo katika shule hiyo.
Barua hiyo inaeleza kwamba "Kumekuwa na taarifa zinazosambaa kupitia kipande cha video clip kinachozunguka katika mitandao ya kijamii zikimuonyesha mtu mmoja akitembelea shule ya msingi Nzasa akiwa amevaa mavazi yaliyo kinyume na maadili ya Kitanzania"
"Tunapenda kutoa taarifa kwamba uongozi wa manispaa ya Temeke umechukizwa na ugeni huo pia hauhusiki kwa namna yoyote juu ya mualiko wa mgeni huyo"
"Aidha uongozi wa Manispaa ya Temeke umemuonya Mkuu wa shule kwa kukiuka maadili ya utumishi wa umma kutokana na kitendo kilichotokea, uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wote uliojitokeza"