Jumamosi , 27th Sep , 2014

Staa wa filamu hapa Bongo, Vicent Kigosi ama Ray kwa jina maarufu, ametoa angalizo juu ya kuibuka kwa wingi kwa Watayarishaji wa Filamu ambao wamekuwa hawazingatii viwango vya ubora wa kazi na hivyo kuharibu soko la sanaa hiyo.

Vicent Kigosi - Ray

Ray akiwa kama msanii mwenye mafanikio tayari, amesema kuwa, sanaa hiyo inaendelea kukuwa isipokuwa, Watayarishaji filamu hawa wameongezeka sana na kuna umuhimu wa wao kufahamu kuwa bila ubora, wanajiharibia wenyewe.

Staa huyu pia akagusia ujio wa kazi yake mpya inayokwenda kwa jina VIP ambayo kwa nafasi kubwa itagusia swala ya Utalii kwa Wazawa ambao wamekuwa nyuma katika swala hili kazi ambayo itatoka mapema mwezi ujao ikiwa na mastaa wakali kabisa ndani yake.