Kwenye ukurasa wake wa twitter Wakazi ameandika ujumbe akisema kwamba alijua suala hilo tangu wakati wa msiba, lakini alishindwa kuliweka wazi kwani hakuwa kwenye nafasi ya kulizungumzia.
Wakazi alienda mbali zaidi kwa kuzungumzia suala la Fid Q kuweka wazi kilichotokea, na kueleza kuwa huenda Fid Q alishindwa kukaa nalo moyoni lakini hakustahili kulizungumzia, bali angewaachia wana familia.