Jumamosi , 8th Aug , 2020

Msanii wa lebo ya Konde Gang Music Ibraah Tz "Chinga" amesema hawezi kuwa kwenye mahusiano na Jacqueline Wopler kwa sababu anamchukulia kama mama yake japokuwa Harmonize alimpigia pande ili awe nae kwenye mahusiano.

Msanii wa Harmonize Ibraah Tz upande wa kushoto, kulia ni msanii wa filamu Jacqueline Wolper

Akizungumzia suala hilo la kupigiwa pande na Harmonize ili awe kwenye mahusiano na Wolper, Ibraah Tz amesema anamchukulia msanii huyo wa filamu kama mama yake na yeye bado yupo single.

"Ule ulikuwa ni utani tu unajua kuna muda kaka natakiwa ni-enjoy naye, haiwezi kuwa mimi nitoke na Jacquline Wolper yule ni mama yangu ananisapoti kwa hiyo namshuru sana sapoti yake ni kubwa kwangu, bado sina mahusiano nikiwa nayo nitaweka wazi na watu watajua" ameeleza Harmonize 

Zaidi tazama hapa chini kwenye video