Ijumaa , 3rd Feb , 2017

Meneja wa msanii wa bongo fleva Snura Mushi anayefahamika kwa jina la HK amesema jambo lililotokea hivi karibuni nchini Nigeria siyo mara ya kwanza kwa msanii Don Jazzy kupost na kupenda nyimbo ya Chura ya Snura.

 

Akongea kupitia eNewz ya EATV, HK amesema hata Bird Man alishapost video ya nyimbo ya Chura jambo linalomaanisha kuwa wimbo wa Chura ulipendwa na ulikubalika na watu wengi hali iinayoonesha kwamba Snura alifanya ubunifu wa kutosha katika nyimbo ya Chura

Hata hivyo HK amesema kwa sasa wapo katika kufanya mipango mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutafuta kufanya kolabo na Don Jazzy au kujiunga na lebo ya Don Jazzy.