Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tuhamasishe watoto kupenda kusoma - Nikki wa Pili

Jumapili , 28th Aug , 2016

Msanii Niki wa Pili ameitaka jamii kuhamasisha watoto kupenda kusoma, na sio kuwafundisha kujua kusome pekee.

Kwenye ukurasa wake wa Instagram baada ya kuona habari iliyoandikwa na www.eatv.tv iliyosema "Wanafunzi 10,273 shule za msingi hawajui kusoma", Niki wa Pili aliandika ujumbe ambao ulionekana kugusa mashabiki zake huku wakimuunga mkono, ulioitaka jamii kuhamasisha watoto kupenda kujua kusoma.

"Kabla ya kumfundisha mtoto kusoma....kwanza mfundishe utamu wa kujuwa kusoma, raha ya kujuwa kusoma, uzuri wa kujuwa kusoma, kifupi usimfundishe kusoma, mtamanishe kujuwa kusoma, mfanye iwe ndoto yake, then the rest will be history, lets not teach, lets inspire the kids to learn", aliandika Niki wa Pili.

Niki wa pili ambaye pia ni msomi mwenye PhD yake mfukoni, aliendelea kwa kusimulia kile kilichomsukuma yeye kupenda kusoma na pengine ndio sababu ya kumfikisha hapo alipo, na kutueleza kuwa kaka yake ambaye pia ni msanii mwenzake Joh Makini, ndiye aliyemshika mkono na kumuonyesha njia sahihi.

"Nakumbuka Joh Makini ndio mtu alinifundisha kusoma na kuandika hata kabla sijaanza shule, kifupi alinifanya nika fall inlove na kusoma na kuandika, since msukumo ulitoka ndani ilinichukuwa muda mfupi sana", aliandika Niki wa pili kwenye ukurasa wake wa instagram.

Kwa upande wa mashabiki wake walimpongeza kwa ujumbe huo wenye kuigusa jamii, huku baadhi yao wakiandika haya..
Masanjalino: Una akili nyingi sana we braza nitamwambia magufuli akutumie.
scottermike: We jamaa unaakili sana,much respect

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa