Jumapili , 10th Mar , 2019

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Vanessa Mdee, amejibu tuhuma za kutoonekana misibani hivi karibuni, baada ya kudai kuwa amechoshwa na tuhuma hizo zisiszo na msingi.

Vanessa amefunguka kila kitu kwenye ukurasa wake wa instagram, baada ya kuandika ujumbe akisema anajua shughuli za mazishi ni kama ibada, hivyo hakuona haja ya kuweka wazi kuwa alihudhuria ama la, ingawa ukweli ni kwamba alikuwepo kwenye misiba hiyo.

Akiendelea kuelezea juu ya hilo, Vanessa Mdee amesema kwamba kutokana na kile alichokipitia baada ya kupoteza baba na dada yake, anajua uchungu wa kufiwa hivyo hakutaka kutumia matukio hayo kama jukwaa la kujionesha na yeye yupo.

 

Niliona nipotezee lakini naomba niseme once and for all. Misiba na mazishi ni kama ibada, ukishiriki sio habari ya kutangaza kama tamasha. Nimeona watu wanataka kunishikilia bango kama mtu asiyehudhuria au asiyeshiriki katika ibada hizi. Kama unataka kufaham nilikuwepo katika misiba yote ya hivi karibuni lakini sikupenda kutangaza uwepo wangu kutokana na kupitia misiba mizito katika maisha yangu kama watu wengine wengi. Siku ya kesho itakuwa miaka 12 tangu nimpoteze baba yangu mzazi na mwaka huu ni miaka miwili tangu nimpoteze Dada yangu ( mtoto wa kwanza wa baba) i bet you didn’t even know, why? Because I prefer to silently pray for the family and loved ones, I’ve found that only God can bring some relief in these situations. Mtu akifiwa anapitia mambo mengi na anahitaji faraja. Nadhani nimeeleweka. Asanteni na Mungu awatunze wote na familia zenu.

A post shared by VeeMoney (@vanessamdee) on

Hivi karibuni Tanzania imekumbwa na misiba ya watu maarufu kwenye tasnia ya habari na burudani, ikiwemo msanii wa Hip Hop Godzilla, Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba na Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde.