Ijumaa , 1st Feb , 2019

Penzi kati ya msanii Vanessa Mdee na Juma Jux limeonekana kuwa imara na kutokubali kutenganishwa, baada ya Vanesa Mdee kukubali kuwa ukewenza na mwanadada mrembo Huda Monroe.

Hayo yamejidhihirisha baada ya Vanessa Mdee kumtaka Hudah aende nchini Burundi ili wakapeane zamu za kumuhudumia Jux, huku yeye akiwa kwenye show.

Tukio zima lilianza kwa Hudah kusifia sauti ya Vanessa Mdee akimuita 'mke mwenza', na ndipo Vanesa akamjibu kwa kumtaka aende Burundi wakasaidiane majukumu.

Ikumbukwe kwamba Hudah ameshawahi kukiri hadharani kuwa anampenda sana Jux na anatamani siku moja angekuwa naye kwenye mahusiano.

Hudah Monroe