Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vodacom, EATV wawatembelea washiriki Dance 100%

Jumamosi , 16th Aug , 2014

Kampuni ya Vodacom Tanzania pamoja na EATV, leo hii imeanza zoezi la kutembelea washiriki wa shindano ya Dance 100% 2014 katika kambi zao za mazoezi ili kuangalia mchakato wa maandalizi ya makundi haya kuelekea hatua ya robo fainali.

Meneja Mahusiano Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu akiwa (katikati mwenye T-Shirt nyeusi) na kundi la Mazabe Powder katika kambi yao Tegeta Dar es Salaam leo.

Zoezi hili limeanzia huko Tegeta jijini Dar es Salaam, ambapo leo timu hii imekutana na kundi la Mazabe Powder na kujionea jinsi maandalizi yao yanavyokwenda.

eNewz ambayo imefuatilia zoezi hili kwa karibu, imeweza kuongea na Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bwana Matina Nkurlu ambaye amesema kuwa zoezi hili ni kwa ajili ya kuwahamasisha washiriki kuitumia nafasi hii kwa nguvu na nia moja ikiwa kama fursa ya ajira pia, na kuwahakikishia kuwa Vodacom ipo nao bega kwa bega.

Vilevile muwakilishi wa kundi la Mazabe Powder, Francis Charles ama Dogo JJ akazungumza na kutoa shukrani zake kwa Vodacom na EATV kwa nafasi hii na kuweka wazi kuwa wamewekeza jitihada za kutosha kuleta ushindani mkubwa katika mashindano haya mwaka huu.

Zoezi hili litaendelea tena siku ya kesho kuyafikia makundi mengine yanayoshiriki Dance 100% 2014 katika kambi zao.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali