Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

WAKALI SISI VINARA DANCE 100% 2014

Jumamosi , 4th Oct , 2014

Fainali ya mashindano makubwa kabisa ya kudansi Afrika Mashariki, Dance 100 2014, yamefanyika leo kwa mafanikio makubwa na kundi la Wakali Sisi kufanikiwa kuibuka kidedea katika nafasi ya kwanza kama wakali wa kudansi kwa mwaka huu.

Kundi la Wakali Sisi Likikabidhiwa Hundi pamoja na Kombe na zawadi zao na Meneja Uhusiano wa Umma kutoka Vodacom, Bwana Matina Nkurlu

Kundi hili limekabidhiwa hundi ya shilingi Milioni 5 kama zawadi kuu ya mshindi, Smartphone aina ya Vodaphone zikiwa na muda wa maongezi shilingi Laki 1 kwa kila mwanakundi, pamoja na Kombe, huku mshindi wa pili The WT akiondoka na hundi ya shilingi Milioni 1 na laki 5, na mshindi wa tatu kundi la Wazawa Crew akiondoka na zawadi ya hundi ya shilingi laki 5.

Hii ni baada ya mpambano mkali wa round mbili kwa kila kundi, hatua ya kwanza ikihusisha kucheza Mega Mix za makundi ana ya piali ikihusisha kucheza nyimbo maalum ambazo ziliandaliwa na waratibu na makundi haya kujichagulia yenyewe.

MAshindano haya pia yamehusisha burudani ya aina yake ambapo katika hatua ya Ufunguzi, washiriki wote walipata nafasi ya kudansi na Msanii Mahiri na mwalimu wa Dansi Msami, kbla ya msanii huyu na timu ya madansa wake kulishambulia jukwaa kwa ku-perform nyimbo zake zinazofanya vizuri ikiwepo Soundtrack.

Vilevile baada ya mzunguko wa pili mkali wa kusuka mabiti na msanii Mesen Selekta naye alilishambulia jukwaa na kufanya live hits zake kali kabisa ikiwepo Kanyaboya.

Majaji wa mashindano haya kama kawaida walikuwa ni Super Nyamwela, Lotus kutoka EATV na Queen Darleen, na washereheshaji wakiwa ni T Bway pamoja na msanii wa muziki mkali kabisa Meninah.

Mashindano haya kwa ujumla wake yamewapambanisha makundi 5, wakiwepo Wakali Sisi, The Winners, Wazawa Crew, The WT pamoja na Best Boys yakidhaminiwa kwa nguvu na Vodacom Tanzania pamoja na Grand Malt.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa