Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Washiriki Dance100% wafunzwa matumizi ya mitandao

Alhamisi , 22nd Sep , 2016

Kampuni ya mtandao wa simu za mikononi nchini Tanzania, Vodacom leo imetoa elimu juu ya matumizi sahihi ya simu kwa washiriki wa fainali za shindano la Dance100% 2016 katika makao makuu ya Vodacom Jijini Dar es salaam.

Meneja wa idara ya huduma kwa wateja Vodacom , Willynevilline Msamo, akitoa maelezo kwa wawakilishi wa makundi yanayoshiriki fainali ya Dance100%

Akizungumza na washiriki hao ambao wametembezwa katika vitengo mbalimbali vinavyohudumia wateja wa kampuni hiyo, Meneja wa idara ya huduma kwa wateja Vodacom , Willynevilline Msamo amesema watumiaji wa simu wanatakiwa kuwa makini hasa katika lugha pamoja na kutuma na kupokea fedha kwani tatizo lolote likitokea ni rahisi kwa mhusika kupatikana.

'Tuzitumie simu zetu na mtandao wa Vodacom kwa manufaa mazuri, tusitukane watu tukidhania hatuwezi kupatikana au kuiba kwa kutumia mtandao , tukiamini tutakuwa salama, malalamiko yakitufikia ni rahisi sana kukupata sehemu ulipo” Amesema Msamo.

Wakati huo huo Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu amewataka vijana wanaoshiriki shindano hilo kutokukata tamaa kwani , juhudi na malengo ndiyo chanzo kikubwa cha mafanikio katika maisha.

Kwa upande wa mmoja wa waratibu wa shindano hilo kutoka EATV Brendansia Kileo amesema maandalizi ya shindano hilo yamekamilika watu wajitokeze kwa wingi siku ya Jumamosi hii, tarehe 24 viwanja vya Don Bosco Osterbay Jijini Dar es Salaam kuanzia saa nne asubuhi.

Aidha kwa upande wake Afisa Msaidizi wa Bidhaa na Masoko kutoka kampuni ya Coca- Cola Mariam Senziga amesema kampuni ya Coca -Cola inafurahishwa namna vijana wanavyojituma katika sanaa na kusisitiza kuwa kampuni hiyo itaendelea kusapoti mawazo chanya yanayoibua vipaji.

Shindano la Dance100% 2016 linafikia tamati kwa mwaka huu Jumamosi ambapo matukio yote yanaoneshwa na EATV pekee kila Jumapili saa moja jioni na kudhaminiwa na Vodacom na Coca- Cola.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi