Jumapili , 15th Feb , 2015

Katika kipindi hiki ambapo tunaelekea katika tukio kubwa la uchaguzi mkuu wa viongozi wa nchi, wasanii mbalimbali wameendelea kutoa mitazamo yao kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa.

Young Killer

Miongoni mwa wasanii hao ni Rapa Young Killer ambaye ametaka wananchi kuwafuatilia kwa makini viongozi hawa ili kuweza kufahamu wale watakaofaa kupatiwa nafasi za uongozi.

Killer ambaye tayari ameonesha uwezo mkubwa katika game ya muziki licha ya umri mdogo alionao, amesema kuwa kila mwananchi anahitaji maendeleo na njia pekee ni kutoa nafasi ya kusikiliza sera na pia mikakati yao wakati ukifika, ili kuweza kufanya maamuzi sahihi.