Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Hatutoi mikopo kwa kuangalia jina la chuo - Wizara

Alhamisi , 1st Dec , 2016

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa serikali haitoi mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa kuangalia jina la chuo au ubaguzi wa wanafunzi.

Mhandisi Stella Manyanya akiwa Kikaangoni

 

Ametoa kauli hiyo katika ofis za EATV wakati akijibu maswali ya wananchi kupitia kipindi cha KIKAANGONI kinachoruka kila Jumatano kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV.

Alilazimika kutoa kauli hiyo kutokana na malalamiko kutoka kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kampala tawi la dar es Salaam walioandamana hadi ofisi za wizara hiyo wakilalamika kukosa mikopo kwa madai kuwa mikopo hiyo inatoka kwa ubaguzi wa kivyuo.

Naibu Waziri huyo amesema kuwa wanafunzi hao wanapaswa kufuata taratibu za kufahamu ni jinsi gani mikopo hiyo inavyotolewa na wafuate utaratibu wa kutoa malalamiko na serikali itaweza kuyachukulia kama changamoto na kuyatatua.

 

Kuhusu madai ya wanafunzi hao, Manyanya amesema amewasikiliza na kubaini kuwa kuna baadhi yao wana hoja za msingi ikiwemo kuwa na vigezo kama vile uyatima na kozi za vipaumbele, lakini akawataka watafute viambatanisho vya ushahidi wa vigezo vyao, na kisha wafuate taratibu za kukata rufaa kupitia Bodi ya Mikopo.

Katika hatua nyingine Mhandisi Manyanya amewataka viongozi wa vyuo mbalimbali wasikilize kero za wanafunzi wanaowaongoza na kuzipeleka sehemu husika na siyo kufanya mgomo na maandamano jambo ambalo haliwezi kusaidia katika utatuzi wa kero zao.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ