Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Facebook na ujio mpya wa huduma ya mahusiano

Ijumaa , 6th Sep , 2019

Facebook wameanzisha huduma mpya, maalum kwaajili ya kuanzisha mahusiano ya ukaribu zaidi baina ya watumiaji wa mtandao huo kama mapenzi na mengineyo.

Huduma hiyo tayari imeanza kupatikana katika nchi kadhaa kama Marekani, Colombia, Thailand na inatazamiwa kuanza kusambaa katika nchi nyingine hivi karibuni.

Huduma hiyo kwa sasa inapatikana katika App kuu ya Facebook hivyo mtumiaji kama unataka kujiunga, itakupasa kuunda wasifu (profile) yako nyingine na utaanza kuona marafiki kadhaa ambao wataanza kuonekana kutokana na mfanano wa taarifa mlizoweka.

Kupitia Instagram pia kipengele hicho kitaongezwa na kupewa jina la "Secret Crush", ambayo itakupa uwezo wa kuwaorodhesha marafiki zako wote kadhaa kwa siri ambao unawapenda na wao wakikubali ombi au kukuorodhesha basi mnaweza kuanzisha uhusiano wenu mnaokusudia.

Mtandao wa Facebook kwa siku za hivi karibuni umekuwa ukituhumiwa kuvujisha taarifa za watumiaji wake hivyo uanzishwaji wa huduma hiyo wachambuzi mbalimbali wa masuala ya mitandao wanaona huduma hiyo usalama kwa watumiaji unaweza ukawa sio rafiki sana.

Facebook kwa upande wao wamesema hawana mpango wowote wa kutumia huduma hiyo kwaajili ya mambo ya kibiashara au kutumia taarifa za watumiaji wake vibaya kama wengi wanavyohisi.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi