Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Janeth asimulia alivyovumilia ukatili kwa miaka 17

Ijumaa , 18th Sep , 2020

Janeth Masawala ameiasa jamii kuhakikisha inamjengea mtoto wa kike uwezo wa kujihami na kuweza kujua namna ya kukabiliana na ukatili ikiwemo vipigo ndani ya ndoa, vitakavyoleta athari kimwili na hata kiafya, kama ambavyo yeye aliathirika na kuwa na kansa ya koo sababu ya vipigo.

Janeth Masawala, mwanamke aliyepitia ukatili wa vipigo kwa mume wake

Janeth ametoa kauli hiyo hii leo Septemba 18, 2020, kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio wakati akisimulia namna alivyoweza kuvumilia vipigo ndani ya ndoa yake kwa kipindi cha miaka 17.

"Tulifunga ndoa mwaka 1998 baada ya wiki tu vipigo vikaanza, nilikuwa napigwa mpaka nazimia kuna kipindi alinipiga kidogo mimba ya mwanangu wa kwanza ikataka kuharibika, unakuta ana visababu vingi mfano mbona mboga ina mafuta", amesema Janeth.

Aidha Janeth akielezea namna alivyopata saratani amesema kuwa, "Ndoa ilinisababishia nipate vipigo na kutokana na vile vipigo kwa muda mrefu ikapelekea goita kuvimba na baadaye kugundulika nina saratani, madhara ya vipigo ni mengi wako wanaopata presha lakini mimi imenipelekea kupata saratani", amesimulia Janeth.

"Nakumbuka tukio jingine, nilipigwa halafu nikafungiwa ndani wiki nzima bila msaada na nilivyokuja kuzinduka nikawa kama chizi, na kwa vile sikuwa sawa nikajikuta nimekunywa pombe kali nikazima kwa siku tatu tena", amesimulia Janeth.

Janeth Masawala kwa sasa ni mwanaharakati wa kutetea haki za wanawake, ambapo amewaomba wanawake wanaopitia ukatili wasijifungie ndani na badala yake watoke kutafuta msaada.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali