Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Madhara ya kujichubua kwa watumiaji

Jumanne , 25th Sep , 2018

Watu wengi hususani wanawake hupenda kuonekana wakiwa warembo, huku miongoni mwao wakiwa na dhana potofu ya kwamba ili uwe mrembo ni lazima ung'arishe rangi ya ngozi yako(Ujichubue).wapo wale wenye usemi ya baadhi ya wanaume kupenda wanawake weupe tamaa ambazo hupelekea-

Pichani ni ngozi iliyoathirika na vipodozi.

shinikizo la wanawake hao kutafuta vipodozi vya kupunguza weusi.

VIPODOZI VINAVYOTUMIKA KUJICHUBUA...

Vipodozi hivi huja katika aina tofauti,Wapo wanaotumia mafuta au dawa ya kung'arisha ngozi zao (lotion) au kumeza tembe. Au kama linavyojulikana kwa jina la Mkorogo. Suala hili linanipa motisha ya kulizamia kwa kina kujua athari za matumizi ya madawa ya kubadilisha ngozi ama kujichubua. (skin bleaching)

 KEMIKALI SUMU NDANI VIPODOZI...

Katika bidhaa zinazotumika kujichubua, kuna kemikali za aina mbili. Ambayo ni ‘Hydroquinone’ na ‘Mercury’
Hydroquinone kemikali hii ni sumu kali, ambayo hutumika kwa ajili ya kuchapisha picha na kutengeneza bidhaa za mpira. pia kama kisaidizi katika kutengeneza rangi za nywele. Mercury nayo ni kemikali ya sumu inayoweza kuuzwa katika maduka ya madawa.

 MADHARA YA KUJICHUBUA...

Katika kujichubua yapo madhara mbalimbali yanayowakumba watumiaji wa vipodozi hivyo;

Dkt. Elizabeth Kilili, ni mtaalamu na Mkurugenzi Mtendaji wa Grace Product Limited ambaye ameainisha madhara yatokanayo na matumizi ya vipodozi hivyo ambayo ni pamoja na kupata kansa ya ngozi, kuzeeka mapema,kupata watoto wenye kasoro, mishipa ya fahamu,figo, kupungua kwa uzito na kupelekea athari za kuvunjika mifupa.Madhara haya huoneka mara moja na kadri mtu anavyozidi kutumia mkorogo kung'arisha ngozi yake.

Pia Dkt Kilili amesema, _“__upande wa mama mjamzito vipodozi venye viambata sumu vina muathiri mtoto kwenye mfumo wake wa chakula kupitia kitovu cha mama, kwa sumu inavyopita huelekea kwenye damu ambayo mtoto anapokuwa anazaliwa hutoka na kasoro tofauti ambazo huleta madhara katika ukuaji wake.”_

USHAURI WA KUZINGATIA...

Dkt Kilili anaendelea kwa kutoa ushauri wa kuepukana na madhara ya kujichubua huku akishauri matumizi ya bidhaa za asili zisizokuwa na madhara, ikiwemo kutumia vipodozi vilivyopitishwa na Mamalaka ya Chakula na Dawa (TFDA) pamoja na kupata ushauri kwa wataalamu juu ya afya na magonjwa ya vipodozi ikiwemo kujikinga na madhara yanayoweza kupelekea athari katika mwili wako.

Msikilize hapo chini Dkt. Kiili akielezea madhara ya kutumia vipodozi vyenye madhara.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa