Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara ajibu kuhusu kuondoka 'Karantini'

Ijumaa , 27th Mar , 2020

Afisa Habari wa Simba, Haji Manara amezungumzia kuhusu kitendo chake cha kuhudhuria mazishi kabla ya siku 14 za kujitenga kutokana na tishio la virusi vya Corona.

Haji Manara

Jana Machi 26, 2020, Manara alihudhuria mazishi ya aliyekuwa Msemaji wa klabu hiyo,  Asha Haji aliyefariki Machi 25 katika hospitali ya Hindu Mandal Jijini Dar es Salaam, ambapo alitokea katika Karantini yake ambayo aliiandaa mwenyewe kwa siku 14 baada ya kurejea nchini akitokea katika ziara yake barani Ulaya.

Katika ukurasa wake wa Instagram, Manara amesema kuwa yeye hana maambukizi ya virusi vya Corona baada ya kupima mara mbili hapa nchini na aliamua kujiweka Karantini kwa hiyari yake, hivyo hajakatazwa kuhudhuria shughuli yoyote.

"Wapo watu wananilaumu eti kwanini nimeenda msibani wakati nipo katika Karantini?. Niwafahamishe ni mimi binafsi kwa hiyari yangu niliamua kukaa Karantini baada ya kutoka safari bila kushurutishwa na yoyote!", amesema Manara.

"Agizo la Mh Rais la kuwataka wote wanaorejea kutoka nje kukaa Karantini kwa siku 14, limetolewa mimi nikiwa tayari nimesharejea, nilipimwa mara mbili hapa nchini na kubainika nipo salama lakini nikasema ngoja nikae mwenyewe kidogo kujisikilizia. Sasa kwa msiba wa dada yangu na kwa kuwa nipo salama baada ya vipimo vya kitabibu kuonyesha hivyo, sikuweza kukaa ndani tena", ameongeza.

Manara pia amesema kuwa watu wanaomlaumu ni wale ambao wanamuombea mabaya ili asifanikiwe.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil