Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mjamzito anavyomsababishia ugonjwa wa akili mtoto

Ijumaa , 14th Sep , 2018

Dkt. Ruchius Philbert ambaye ni Afisa Muuguzi kutoka hospitali ya Taifa ya Muhimbili, mtafiti pia mkufunzi wa masuala ya afya ya akili, amesema katika sababu zinazochangia matatizo ya afya ya akili, mama mjamzito ni kisababishi kikuu kwa mtoto aliye tumboni.

Mwanamke mwenye ujauzito

Akizungumza katika kipindi cha SUPAMIX cha East Africa Radio leo, Philbert amesema mama mjamzito asipofuata kanuni za ulaji kwa wakati ikiwemo lishe duni, ni sababu kuu kupelekea mtoto kuzaliwa akiwa na matatizo ya akili au kumpata baadaye ukubwani.

''Tafiti mbalimbali zimefanyika na kuonesha hakuna chanzo kimoja cha ugonjwa wa akili, lakini lishe duni kwa mama mjamzito ni sababu pekee kubwa kupelekea mtoto azaliwe na tatizo la afya ya akili, kwani malezi ya mtoto huanzia tumboni mwa mama, na matokeo yake ni mtoto kuwa na utindio wa ubongo'', ameeleza Dkt. Philbert.

Aidha, Dkt. Philbert amezitaja sababu kuu tatu ambazo husababisha mvurugikano wa afya ya akili, ambazo ni za kibailojia ikiwa ni njia ya kurithishana 'vina saba' kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, nyingine ni kisakolojia hutokea kama mtu ananyanyapaliwa au kutengwa, na sababu ya tatu ni ya kijamii ambayo uhusisha mazoea ya jamii inayomzunguka mtu, mfano unywaji wa vilevi kupita kiasi ikiwemo bangi, pombe na mifarakano ya kwenye jamii.

Dkt. ameendelea kwa kusema ''dalili za awali za ugonjwa wa akili hazigunduliki kwa haraka sana, ndio maana watu wengi hukumbwa na tatizo hili, hivyo basi sisi kama wataalam tunashauri mtu  kuonana na wataalam
wa masuala ya akili mara kwa mara kwa ajili ya ushauri tiba''.

Kila mwaka tarehe 10, Oktoba hufanyika maadhimisho ya Afya ya Akili duniani kote, mwaka jana 2017 nchini Tanzania katika maadhimisho hayo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alitoa takwimu kutoka Shirika la Afya duniani (WHO)zinaonyesha mmoja kati ya watu wanne alishapata au alishaona mtu mwenye matatizo ya kiakili.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa