Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Rais Magufuli ni mkali sana'' - Wahadzabe

Jumanne , 18th Jun , 2019

Baada ya muda mrefu, hatimaye Jamii ndogo ya kabila la Wahadzabe ambao kwa asili husishi mapangoni na chini ya mibuyu mikubwa imeanza kutambua umuhimu wa watoto wao kupata elimu.

Baadhi ya wanajamii wa kabila la Wahadzabe

www.eatv.tv kupitia kwa mwandishi wake Dotto Kadoshi, imewatembelea wananchi hao waishio katika Bonde la Eyasi wilayani Karatu mkoani Arusha ambapo wameeleza kuwa wameelewa kuwa elimu itawasaidia, kukabiliana vyema na mabadiliko ya tabia nchi ambayo tayari yameonekana kuanza kuathiri mfumo mzima wa maisha yao ya asili.

Jamii hiyo ambayo kwa asili, pamoja na kuishi mapangoni au chini ya mibuyu mikubwa lakini pia huendesha maisha yao kwa kuwinda, kuokota matunda, kuchimba mizizi porini na kula nyama mbichi hususani ya nyani, sasa wameanza kubadili mtazamo wao wa kifikra juu ya elimu kwa watoto wao.

Hata hivyo Jamii hiyo imeonesha wasiwasi wake wa kushindwa kutekeleza baadhi ya majukumu yake ya asili ya kila siku kutokana na kuingiliwa maeneo yao na baadhi ya jamii nyingine.

Asili ya Jamii ya kabila la Wahadzabe inaelezwa ni Afrika Kusini, ambapo katika harakati zao za uwindaji na kusaka matunda maelfu ya miaka iliyopita waliingia Tanganyika kupitia misitu ya Kongo.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa