Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali imeombwa kuondoa kodi ya taulo za kike

Alhamisi , 16th Jun , 2022

Kampeni ya Namthamini ya East Africa Television na East Africa Radio katika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika Duniani, leo ilifika katika shule ya sekondari Turiani kuzungumza na wanafunzi na kugawa taulo za kike.

wanafunzi wa Turiani wakifurahi baada ya kukabidhiwa taulo za kike za mwaka mzima.

Wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu wapatao 59 wamepatiwa pakiti 716 za taulo za kike zitakazowasaidia kutumia kwa mwaka mzima.

Mratibu wa Kampeni ya Namthamini, Millicent Lema Lasway amesema lengo la kampeni hiyo kufika katika shule hiyo ni kutoa elimu ya hedhi, ambayo ni lazima itolewe kwa watoto wa kike na kiume, na ikiwa ni siku ya Mtoto wa Afrika Duniani ni vyema kuvunja ukimya na kutoa elimu ya afya kwa watoto.

''Tunashukuru kuona watoto wa kiume wamejitokeza, kwa sababu kampeni yetu licha ya kumsaidia mtoto wa kike pia inalenga kuvunja ukimya juu ya hedhi.'' alisema Millicent Lasway

''Maisha yanabadilika na vijana tunajifunza vitu vingi, sio kitu cha ajabu ndiyo maana tukapenda watoto wa kiume wawepo" aliongezea Millicent Lwasay

Pia Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari Turiani, Projestus Barongo amaeiomba serikali kuondoa kodi katika taulo za kike ili kuwawezesha watoto wa kike kuwa huru wawapo katika siku za hedhi.

Kampeni ya Namthamini imeingia msimu wa sita mwaka huu, zoezi la uchangiaji linaendelea na wadau wanaombwa kuchangia kampeni hii ili kusaidia na kuinua kiwango cha elimu nchini kwa watoto wa kike ambao hukosa masomo kwa zaidi ya siku 50 kwa mwaka.

Hii ni shule ya tano iliyofikiwa na Kampeni ya Namthamini tangu izinduliwe Mei 27 mwaka huu.

 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ