Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ujumbe wa mwisho wa rubani kwa mama yake

Alhamisi , 14th Mar , 2019

“Narudi nyumbani Nairobi, nimeshau simu yangu hotelini, tutaongea zaidi nikifika huko”.

Haya ni maneno ya mwisho ya Yared Tessema Getachew, rubani kijana aliyekuwa akirusha ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia, iliyopata ajali mwishoni mwa wiki iliyopita na kuua watu 157 waliokuwemo

Maneno hayo alimwambia mama yake mzazi kwa kumtumia ujumbe wa simu, kabla ya kurusha ndege hiyo ya Boeing 737 Max 8, asubuhi ya Jumapili ya Machi 10, 2019.

Yared mwenye miaka 29 alikuwa ni raia wa Kenya, ndiye aliyekuwa rubani mkuu kwenye ndege hiyo iliyosababisha vifo vya mamia ya watu.

Mpaka sasa mwili wa rubani huyo bado haujapatikana, ili kufanyiwa mazishi kwa imani yake ya dini ya kiislam.

Baba wa rubani huyo Dr. Getachew Tesema,  amesema mtoto wake alikuwa mwenye akili sana darasani na alikuwa akipenda kuogelea, mpaka marafiki zake walimpa jina la 'Mr. Fish'.

Akiendelea kuelezea machungu yake, Dr. Tesema ameweka wazi kuwa kijana wake huyo mtanashati alikuwa ameshachumbia, na mipango ya ndoa ilikwishaanza.

Baba asimulia

“Alikuwa mchapa kazi na akimuheshimu kila mmoja, mkubwa au mdogo, watu walimpenda sana na kumuheshimu pia, alikuwa ni baraka kwa mambo mengi, na alikuwa karibu sana nami, nilimshawishi aende Ethiopia kwa masomo badala ya Afrika Kusini na kupata kazi kwenye shirika kubwa kama lile, nikatarajia ataleta mabadiliko makubwa sana, sioni kama kuna mtoto ambaye anaweza chukua nafasi yake, alikuwa wa kipekee”, amesema Dr. Tesema.

Akiwa mtoto wa 5 kati ya watoto 6 wa Dr. Tesema, Yared alizaliwa mwaka 1989 nchini Kenya, na mama yake ambaye pia ni daktari.

Baba mzazi wa Rubani Yared, Dr. Tesema

HABARI ZAIDI

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji