Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wasiokula mbogamboga hatarini kuugua magonjwa haya

Jumapili , 20th Jan , 2019

Ni kawaida sana kusikia mtu akiagiza chakula hotelini au mgahawani, akisema kuwa asiwekewe mbogamboga kwasababu tuu hakuzoea kula, wengine wakidai kuwa hawaoni ladha na wengine wakidai kuwa hawajakua katika maisha ya kula mbogamboga.

Mbogamboga na matunda

Inaelezwa kuwa raia wengi wa bara la Afrika hawazingatii ulaji wa virutubisho mbalimbali vya mwili, sababu zikiwa ni umasikini, kukosa elimu ya lishe bora pamoja na uhaba wa mbogamboga katika maeneo mengi hasa yaliyo na ukame.

Mbogamboga na matunda zimesheheni vitamini na virutubisho muhimu sana katika afya ya binadamu. Kwa mujibu wa mtafiti, Laura Moore wa Chuo Kikuu cha Afya cha Texas, hata kama unaweza kupata virutubisho vingi kutoka vyakula vingine, lakini bado mwanadamu anaweza kupata magonjwa mbalimbali kutokana na kukosa virutubisho vitokanavyo na mbogamboga na matunda.

Zifuatazo ni dalili ambazo zinaweza kukuonesha kuwa una upungufu wa vitamini zitokanazo na matumizi hafifu ya vyakula vya mbogamboga na matunda.

Matatizo ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula

Kutopata mbogamboga na matunda ya kutosha kunaweza kusababisha matatizo ya mmeng'enyo wa chakula tumboni kama vile kuganda kwa chakula tumboni (Constipation) na kupelekea ugumu wa mmeng'enyo. Hii ni kwasababu mboga mboga na matunda vina kambakamba ambazo husaidia kuongeza uzito wa kinyesi na kupitisha kwa urahisi.

Hupunguza hatari ya ugonjwa wa Kansa

Kwa mujibu wa Taasisi ya Utafiti wa Kansa ya Marekani (AICR), chakula pekee kinachoweza kupunguza hatari dhidi ya kansa kwa mwanadamu ni lishe iliyosheheni vyakula vya mbogamboga na matunda. vyakula hivyo vinazalisha virutubisho visivyo na sumu kama Vitamin E na Vitamin C ambavyo hupunguza hatari ya kansa.

Kuongezeka kwa hatari ya shinikizo la damu

Mwanadamu akila vyakula vingi vya madini ya sodium bila kuzingatia matumizi ya mbogamboga na matunda hupelekea shinikizo la damu. Utafiti pia unaonesha kuwa mwanadamu mwenye shinikizo la damu anaweza kupunguza kiwango hicho kwa kutumia mbogamboga na matunda zaidi kuliko matumizi ya madawa.

Hupunguza hatari ya magonjwa ya moyo

Pale ambapo shinikizo la damu huwa chini, kula vyakula vya mbogamboga na matunda inaweza kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo na kiharusi yanayoweza kusababishwa na tatizo hilo. Mboga mboga na matunda havina 'Cholesterol' kwahiyo kutumia sana vyakula hivi humsaidia mtu kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo na kiharusi.

Kuongezeka kwa uzito

Kutojali vyakula vya mbogamboga na majani pia kunasababisha mwanadamu kuongezeka uzito kwasababu atakuwa anatumia vyakula vyenye mafuta na kalori. Vyakula vya mbogamboga na matunda havina mafuta na kalori kwahiyo endapo mtu atazingatia zaidi katika mlo wake, atakuwa salama zaidi katika kuzuia kuongezeka kwa uzito.
 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi