Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu wenye ulemavu, S/Mtaa watupiana mpira

Alhamisi , 26th Sep , 2019

Watu wenye ulemavu wanaoishi maeneo ya Mzimuni, Kawe Jijini Dar es Salaam wameilalamikia serikali ya mtaa huo kuwaandikisha majina kwa ajili ya kupata msaada wa vitendea kazi na usafiri wa bajaji ili kujikwamua kibiashara lakini wanaishia kudanganywa.

Pili Adam

Wakizungumza na EATV & EA Radio Digital, wananchi hao wamesema kuwa Serikali ya mtaa imekuwa ikiwafuata na kuwaandikisha majina ili wapewe bajaji lakini mwisho wa siku wamekuwa wakiachwa kwenye vikao vya mwisho vya maamuzi ilhali wao ni wahusika wakuu.

"Serikali yetu ya mtaa inaishia kutuandikisha tu majina na kutuambia mtaletewa msaada lakini vikitokea vikao vya walemavu wanaenda wao wazima, walemavu wa Kawe wote masikini hakuna mwenye nafuu hata mmoja",  amesema Pili Adam ambaye ni moja ya watu wenye ulemavu wanaoishi mtaa huo.

Aidha, Pilli Adam ameongeza kuwa msaada mkubwa ambao utawasaidia wao ni kupatiwa bajaji, zitakazowawezesha katika usafiri na hata kujipatia kipato tofauti na kupewa pesa mkononi.

Hata hivyo EATV&EA Radio Digital imemtafuta Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mzimuni, Hassan Ngonyani ambaye amekanusha taarifa hizo na kusema.

"Mimi hiki kitu sikijui kabisa, mimi nilishawagawiaga maeneo kwa ajili ya uzalishaji mali ili waweze kujipatia rizki lakini wameuza yale maeneo", ameeleza Mwenyekiti wa mtaa huo. 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali