Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Abdi Banda kuhusu kuhusishwa na virusi vya Corona

Jumatano , 18th Mar , 2020

Mlinzi wa klabu ya Highlands Park ya nchini Afrika Kusini na timu ya taifa ya Tanzania, Abdi Banda amezungumzia tetesi kuhusu kukumbwa na virusi vya Corona.

Abdi Banda

Banda ametoa taarifa hiyo baada ya tetesi mbalimbali kusambaa katika mitandao ya kijamii zikimuhusisha mlinzi kukumbwa na virusi vya Corona na kupelekea kutengwa na timu yake ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida.

Kupitia mtandao wa Instagram, Banda amekanusha taarifa kuhusu kukubwa na virusi vya Corona, ambapo amesema, "napenda kutoa shukrani zangu kwa wote mlioguswa/shtushwa na habari juu yangu, kikubwa kila kitu kimeenda sawa".

"Kwa baraka za Mwenyezi Mungu imegundulika haukuwa ugonjwa unaosumbua kwa sasa duniani (virusi vya Corona). Ahsanteni sana MUNGU awabariki", ameongeza.

Abdi Banda aliitwa katika kikosi cha timu ya taifa Taifa Stars, kilichokuwa kikijiandaa na mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya AFCON dhidi ya Tunisia lakini hakuwasiri kambini, hali iliyozusha wasiwasi huo.

Hata hivyo mchezo huo uliahirishwa na Shirikisho la Soka barani Afrika CAF kutokana na tishio la kusambaa kwa virusi vya Corona.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa