Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Achana na matokeo, Man United yakimbiza Ulaya

Alhamisi , 11th Oct , 2018

Suala la matokeo limekuwa ndiyo gumzo kubwa hivi sasa kwa klabu ya Manchester United, ambapo mpaka sasa imeshinda michezo minne pekee katika ligi msimu huu, ikipoteza michezo mitatu na sare moja.

Si msimu huu pekee, hata katika misimu kadhaa ya nyuma tangu aondoke Sir Alex Ferguson, klabu hiyo imekuwa haifanyi vizuri katika michuano yote inayoshiriki ukiondoa msimu uliopita ambapo ilimaliza nafasi ya pili katika ligi. Lakini swali ambalo unaweza kujiuliza, ni kwanini inaendelea kulipa mishahara na kusajili wachezaji wa bei kali duniani?.

Fahamu hapa kuwa Manchester United ndiyo klabu pekee yenye wadhamini wengi kuliko klabu zote barani Ulaya, ina jumla ya wadhamini 68 ambao huchangia faida ya takribani Pauni 269 millioni kwa mwaka kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2018 iliyotolewa na kampuni ya masuala ya michezo na burudani ya CSM.

Hiyo ndiyo sababu klabu hiyo inaendelea kuwa na nguvu zaidi nje ya uwanja licha ya changamoto zote inazozipitia katika miaka hii ya karibuni. Klabu zingine zinazofuatia kwa mujibu wa ripoti hiyo ni pamoja na, Barcelona inayoingiza Pauni 261 millioni kwa idadi ya wadhamini 43, Bayern Munich yenye wadhamini 29 ambayo inavuna jumla ya Pauni 180 millioni na Real Madrid katika nafasi ya nne, ikiwa na wadhamini 19 ambao wanaipa jumla ya Pauni 178 millioni kwa mwaka.

Nafasi ya tano ikishikiliwa na Chelsea yenye wadhamini 18 ambao huiingizia klabu hiyo jumla ya Pauni 154 millioni, nafasi ya sita ni Manchester City, ya saba ni Arsenal huku nafasi ya nane, tisa na ya kumi zikishikiliwa na Liverpool, PSG na Juventus.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa