Senzo Mbatha na Haji Manara
Kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter, Senzo ameandika ujumbe wa kuushukuru uongozi wa klabu hiyo kwa nafasi ambayo umempa kuiongoza klabu na kujivunia mafanikio yaliyopatikana katika kipindi kifupi.
A special thank you message to @SimbaSCTanzania leadership for providing me the opportunity to lead this great club. I regrettably have tendered my resignation from the club with immediate effect. Within a short space of time , a lot has been achieved. Asanteni Sana wana Simba.
— Senzo Mbatha (@SMbatha_Senzo) August 9, 2020
Senzo alijiunga mwaka uliopita ndani ya klabu hiyo na kujizolea sifa nyingi za kiuongozi pamoja na kuisaidia klabu kushinda mataji matatu msimu wa 2019/20 ikiwa ni pamoja na Ligi Kuu Tanzania bara, Kombe la Shirikisho (ASFC) na Ngao ya Jamii.
Pia katika msimu wake wa kwanza, Simba ilifanikiwa kuvuka hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika baada ya kufanya vizuri katika michezo ya kundi lake.