Jumatatu , 22nd Mar , 2021

Xavi Alonso anatarajiwa kutangazwa rasmi kuwa kocha wa Borussia Monchengladbach muda wowote kuanzia sasa, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Marco Rose ambaye msimu ukiisha anatajiunga na na majirani zao Borussia Dotmund

Xabi Alonso anatarajiwa kutangazwa kuwa kocha wa Borussia Monchengladbach

Alonso ambaye ni kiungo mchezeshaji wa zamani wa Liverpool, Real Madrid na Bayern Munich  wamekubaliana vipengele vyote muhimu ili kujiunga na timu hiyo ya Monchengladbach kilichobaki ni kutangwaza tu.

Kwenye eneo la ukocha Alonso hajakuwa na uzoefu mkubwa katika nafasi hiyo, kwa sasa alikuwa kocha wa kikosi cha pili cha klabu ya soka ya Real Sociedad anakwenda kuiongoza timu ya ligi 'bundesliga' yenye ushindani mkubwa

Alonso kiungo fundi aliyewavutia mashabiki wengi duniani akiwa mchezaji, huwenda akapoteza heshima yake kwenye eneo hili la ukocha kama hata pata mafanikio, wadadisi wa mambo wanaona klabu ya Monchengladbach walipaswa kuajiri kocha mwenye uzoefu ili angalau waweze kufuzu mashindano ya Ulaya

Pamoja na Xavi kujiunga ana timu hii mahususi kwa msimu ujao, kwa sasa Moenchengladbach ipo kwenye nafasi ya 10 katika msimamo wa ligi wenye timu 18 huku ikiwa na alama 36 katika michezo 26