Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Aslay kunogesha robo fainali Bball Kings

Ijumaa , 20th Jul , 2018

Kamati ya mashindano ya Sprite Bball Kings kupitia kwa mratibu wa mashindano Yohana Komba, imesema kila kitu kipo sawa kuelekea mechi za robo fainali ya michuano hiyo kesho Julai 21.

Msanii Aslay

Komba amesema tofauti na mechi za hatua zilizopita, robo fainali itanogeshwa na mambo mbalimbali ikiwemo burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wa Bongofleva  ambao watakuwepo kuunga mkono timu wanazozishabikia. 

''Kesho mambo yatakuwa vizuri sana kwanza burudani ya kinywaji baridi cha Sprite ambao ndio wadhamini wetu lakini msanii Aslay pia atakuwepo na wengine bila kusahahu zawadi kwa mashabiki watakaohudhuria'', - amesema.

Kwa upande wao shirikisho la Kikapu Tanzania (TBF),  kupitia kwa kamishna wa ufundi na mashindano Manase Zabron, ameeleza kuwa waamuzi wamejiandaa vizuri kuhakikisha wanachezesha kwa usawa na haki ili anayestahili kwenda mbele aende.

Mechi za kesho zitaanza saa 6:00 mchana hadi saa 2:00 usiku kwenye uwanja wa ndani wa taifa. Dimba litafunguliwa na timu za Water Institute  Vs Flying Dribblers huku Team Kiza dhidi ya DMI kabla ya mabingwa watetezi Mchenga Bball Stars kuvaana na St. Joseph na Temeke Heroes Vs Portland.

Timu ya Portland

Washindi wanne wa kesho watatinga hatua ya nusu fainali kabla ya timu mbili kuingia fainali tayari kwa kuiwania zawadi nono ya bingwa ambayo ni milioni 10 na mshindi wa pili milioni 3 huku 'MVP' akichukua milioni 2. Njoo tuirudishe heshima ya kikapu Bongo.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali