Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Azam FC kuzawadiwa Mil.75

Alhamisi , 24th Apr , 2014

Mdhamini mkuu wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara Vodacom ametangaza kuipa klab ya Azam FC kitita cha shilingi milioni 75 baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa ligi hiyo msimu huu.

Azam FC wakishangilia goli katika moja ya michezo yao ya ligi kuu ya Tanzania Bara ya msimu uliomalizika

Mdhamini mkuu wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara Vodacom ametangaza kuipa klab ya Azam FC kitita cha shilingi milioni 75 baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa ligi hiyo msimu huu.

Akitangaza zawadi mbalimbali kwa mshindi wa pili Yanga anayepata shilingi milioni 37 wa tatu,timu ya Mbeya City anapata shalingi milioni 26 na ya nne Simba inapata shilingi milioni 21 Meneja Uhusiano wa Vodacom, Salum Mwalimu,ametaja pia zawadi kwa ajili ya wachezaji bora.

Amesema mchezaji bora atavuna Milion 5.2, mfungaji bora pia atapata Milion 5.2, mlinda mlango bora milion 5.2 pia na mwamuzi bora na Mwalimu bora watapata milion 7.8 kila mmoja.

Amesema kuwa Jumla ya zawadi zote kwa msimu huu ni Milion 210 kwa ajili ya timu zilizoshika nafasi nne za juu pamoja na timu nyingine zilizoonesha umahiri katika maeneo mengine ikiwemo timu yenye nidhamu itakayovuna Milion 16.

Mwaka jana bingwa wa Ligi Kuu (Yanga) ilizawadiwa kitita cha shilingi Milion 70.

Salum Mwalimu, amesema ligi ya msimu huu imekuwa na ushindani mkubwa ukilinganisha na msimu uliopita.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya ligi hiyo, Silas Mwakibinga, anasema licha ya changamoto nyingi katika ligi ya msimu huu ushindani ndio jambo la msingi katika maendeleo ya mpira nchini.

Sherehe za kukabidhi zawadi hizi, zitafanyika wiki ya kwanza ya mwezi Mei

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya