Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Azam FC yafuata nyayo za Simba SC

Ijumaa , 20th Jul , 2018

klabu bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC imekuwa timu ya pili kufuata nyayo za mabingwa watetezi wa ligi Kuu Tanzania Bara, Simba SC kutangaza mipango yao kuweka kambi nje ya nchi kuelekea michuano ya ligi kuu inayotarajiwa kuanza Agosti 22, mwaka huu.

Azam FC iliyopo juu kwenye picha huku Simba yenyewe ikiwa kwa chini

Hayo yamebainishwa na Afisa habari wa klabu hiyo, Jaffer Idd Maganga na kusema kwamba lengo kubwa ya safari hiyo ni kutaka kumpa fursa kocha wao mpya Hans Pluijm kuwajua vizuri wachezaji na kuipangilia vizuri timu ili kusudi watakaporejea nchini Agosti 15 wawe tayari wameshajuana vizuri.

"Klabu ya Azam inatarajia kuondoka nchini kuelekea Uganda mnamo Julai 30, ina kwenda huko kwaajili ya mazoezi pamoja na kucheza mechi mbalimbali za kirafiki nchini humo na tunatarajia kurejea Agosti 15", amesema Maganga.

Pamoja na hayo, Maganga ameendelea kwa kusema "safari hii itampa fursa mwalimu Hans kuwajua wachezaji ambao anawafundisha maana hajawahi kukaa nao na vile vile kuweza kutengeneza timu yenye umoja na ushirikiano ambayo itakuja kupambana kwenye ligi kuu na kwa jinsi tulivyosajili basi tunaamini tutapata mafanikio makubwa".

Katika timu zinazoshiriki michuano ya ligi kuu Tanzania Bara, Azam Fc imekuwa ya pili kufuata nyayo za Simba SC kuweka mipango yake hadharani ya eneo ambalo watakuwa wanajifua kuelekea michuano hiyo.

Msimu ulioisha wa ligi kuu Tanzania bara 2017/18, Azam FC ili maliza ligi ikiwa nafasi ya pili kwa alama 58 akifuatiwa na Yanga SC ambaye alikuwa bingwa mtetezi kwa alama 52 huku Simba akishika na nafasi ya kwanza kwa alama 69.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa