Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Azam FC yaziburuza Simba na Yanga kimataifa

Jumatano , 9th Jan , 2019

Farid Mussa, Shaaban Idd, Himid Mao ‘Ninja’ na Yahya Zayd ni wachezaji wanaoipa jeuri Azam FC kuwa miongoni mwa klabu iliyofanya vizuri kwenye kutoa vipaji na kuvipeka kimataifa katika miaka ya hivi karibuni tofauti klabu kongwe Simba na Yanga.

Yahya Zayd

Klabu hiyo imekuwa mfano kwenye suala la biashara ya wachezaji ambapo wengi iliwaruhusu wakati ambao inawahitaji zaidi mfano ikiwa ni Shaaban Idd ambaye aliondoka akiwa mfungaji bora wa timu kwenye michuano ya Sportpesa.

Hivi karibuni Yahya Zayd aliondoka nchini kwenda Misri kufanyiwa vipimo vya afya na klabu ya Ismaily ambapo leo Azam FC imethibitisha kufikia makubaliano na klabu hiyo juu ya mauzo ya mshambuliaji huyo chipukizi.

Zayd mwenye miaka 20, yupo nchini Misri tayari hivi sasa kwa vigogo hao wa soka walioingia hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka huu, ambapo ameshamaliza taratibu zote za kimkataba.

Zayd alikulia kwenye malezi ya soka ya Azam Academy na kupandishwa timu kubwa ya Azam FC msimu uliopita (2017-2018).

Farid Mussa na Shaaban Idd wanaokipiga CD Tenerife ya Hispania, nahodha wa zamani, Himid Mao ‘Ninja’, anakipiga Petrojet ya nchini Misri na sasa ameungana kwenye ligi moja na Yahya Zayd.

Mara ya mwisho mchezaji wa Yanga kwenda nje ni Hassan Kessy aliyekwenda Nkana FC ya Zambia akitanguliwa na Simon Msuva aliyekwenda Morocco huku mchezaji wa Simba akiwa ni Abdi Banda aliyekwenda Baroka FC ya Afrika Kusini.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali